2/25/2016

Uganda na Ulaghai katika Demokrasia

                                    
Siku ya Alhamis  tarehe 18.2.2016 ni moja ya siku iliyokuwa ya kihistoria nchini Uganda,nahiita siku hiyo ya kistoria kwa sababu ya uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo siku hiyo.Ulikuwa ni uchaguzi wa kihistoria kwa sababu mbalimbali; mosi, ni uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa kutokana na wagombea urais yaani wagombea watatu kukubalika mno  na kuwa na ushawishi mkubwa kwa wananchi,na wagombea hao ni Yoweri Kaguta Museveni  wa chama cha NRM,Dk Kiiza Besigye wa FDC na Amama Mbabazi.Pili ni uchaguzi uliotanguliwa na mdahalo wa wagombea urais kipindi cha kampeini  ambapo kila mmoja wao alijieleza nini angefanya kama angepewa ridhaa na wananchi
Ni dhahiri watu wengi walikuwa na shauku ya kutakakjua na kuona jinsi zoezi zima la uchaguzi litakavyoenda,hiyo inaweza kudhihirishwa na vyombo vya habari kutoka ndani na nje jinsi vlivyomulika zoezi zima la uchaguzi  na pia mitandao ya kijamii nayo haikuwa nyuma kuhakikisha watu wanapashana habari  katika zoezi hilo
Naweza kusema ni uchaguzi uliogubikwa na matukio mengi mpaka kutiliwa shaka kwa jinsi zoezi lilivyoendeshwa na mambo mbalimbali yaliyojitokeza kipindi cha uchaguzi huo.Moja ya matukio hayo,ni  jeshi la polisi kutumia nguvu kubwa pasipo sababu ya msingi kwa kuwakamata wananchi na viongozi wa upinzani.Kwa mfano kuna baadhi ya wananchi  na viongozi wa upinzani kama Dk Kiiza Besigye kukamatwa na jeshi la polisi zaidi ya mara mbili na ofisi ya Chama Chake Cha FDC kuvamiwa pasipo sababu za msingi.Tatu ni nyumba za viongozi wa upinzani kama Amama Mbabazi kuzingirwa na jeshi la polisi nyakati tofauti
Hayo ni matukio makubwa yaliyojitokeza katika kipindi hicho cha uchaguzi.Hata hivyo, kuna kasoro mbalimbali zilizojitokeza kipindi hicho,na kasoro hizo ni vituo vya kupigia kura kufunguliwa mapema lakini vifaa vya kupigia kura kutokifa vituoni mapema na kuletwa dakika za mwisho muda wa kupiga kura ukiwa unakaribia kuisha na matokeo ya uchaguzi vituoni kuzidi idadi halisi ya wananchi waliojiandikisha katika vituo hivyo.Kwa hiyo matukio hayo na kasoro hizo zinabaki kuibua maswali mengi kwa watu wengi.
Maswali hayo yanayoibuka ndani ya vichwa vya watu wengi ni kwanini  jeshi la polisi lilitumia nguvu kubwa  kukamata wananchi na viongozi wa upinzani na kuvamia ofisi za vyama vyao  pasipo sababu za msingi na walifanya hivyo kwa malengo yapi na kutumwa na nani?. Na inakuaje kasoro nyingi, mfano namba ya wapiga kura kuzidi namba halisi ya watu waliojiandikisha katika vituo hivyo?Je chombo husika yaani tume hawakuwa wamejiandaa kukabiliana na aina ya udanganyifu wowote, au tume iliamua kufumbia macho kasoro hizo kwa kuweza kukibeba chama kilichokuwa madarakani?
Kama Afrika tumeamua kukubali mfumo wa vyama vingi basi tuwe tayari kukabiliana na matokeo ya mfumo huo,ni dhahiri na imezoeleka kuwa vyama vinavyokuwa madarakani  pale uchaguzi unapokaribia kufanyika matukio mengi yamekuwa yakijitokeza,yaani serikali iliyopo madarakani kutumia kila njia kutaka kushinda uchaguzi kwa kukiuka taratibu na kujenga taswira machoni  mwa watu kwa  vyama vya upinzani  kuonekana kama  chanzo cha vurugu katika chaguzi.
Nafikiri  ifike pahala watawala watambue kuwa vyama vya upinzani vinaweza kuongoza nchi kama wananchi wameamua kuvipa ridhaa,hivyo maamuzi hayo yaheshimiwe kwa sababu wananchi ndiyo wenye nchi na ni jukumu lao kuamua nani atakuwa kiongozi wao, isitumike nguvu kubwa ya chama tawala kutumia nguvu dora kuhakikisha uamzi wa watu unaingiliwa.Tumeamua kuruhusu mfumo wa vyama vingi,hivyo tuwe tayari kukubali matokeo ya mfumo huo.
Chagulani,Shabiru

25.2.2016

Uganda na Ulaghai katika Demokrasia

                                    
Siku ya Alhamis  tarehe 18.2.2016 ni moja ya siku iliyokuwa ya kihistoria nchini Uganda,nahiita siku hiyo ya kistoria kwa sababu ya uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo siku hiyo.Ulikuwa ni uchaguzi wa kihistoria kwa sababu mbalimbali; mosi, ni uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa kutokana na wagombea urais yaani wagombea watatu kukubalika mno  na kuwa na ushawishi mkubwa kwa wananchi,na wagombea hao ni Yoweri Kaguta Museveni  wa chama cha NRM,Dk Kiiza Besigye wa FDC na Amama Mbabazi.Pili ni uchaguzi uliotanguliwa na mdahalo wa wagombea urais kipindi cha kampeini  ambapo kila mmoja wao alijieleza nini angefanya kama angepewa ridhaa na wananchi
Ni dhahiri watu wengi walikuwa na shauku ya kutakakjua na kuona jinsi zoezi zima la uchaguzi litakavyoenda,hiyo inaweza kudhihirishwa na vyombo vya habari kutoka ndani na nje jinsi vlivyomulika zoezi zima la uchaguzi  na pia mitandao ya kijamii nayo haikuwa nyuma kuhakikisha watu wanapashana habari  katika zoezi hilo
Naweza kusema ni uchaguzi uliogubikwa na matukio mengi mpaka kutiliwa shaka kwa jinsi zoezi lilivyoendeshwa na mambo mbalimbali yaliyojitokeza kipindi cha uchaguzi huo.Moja ya matukio hayo,ni  jeshi la polisi kutumia nguvu kubwa pasipo sababu ya msingi kwa kuwakamata wananchi na viongozi wa upinzani.Kwa mfano kuna baadhi ya wananchi  na viongozi wa upinzani kama Dk Kiiza Besigye kukamatwa na jeshi la polisi zaidi ya mara mbili na ofisi ya Chama Chake Cha FDC kuvamiwa pasipo sababu za msingi.Tatu ni nyumba za viongozi wa upinzani kama Amama Mbabazi kuzingirwa na jeshi la polisi nyakati tofauti
Hayo ni matukio makubwa yaliyojitokeza katika kipindi hicho cha uchaguzi.Hata hivyo, kuna kasoro mbalimbali zilizojitokeza kipindi hicho,na kasoro hizo ni vituo vya kupigia kura kufunguliwa mapema lakini vifaa vya kupigia kura kutokifa vituoni mapema na kuletwa dakika za mwisho muda wa kupiga kura ukiwa unakaribia kuisha na matokeo ya uchaguzi vituoni kuzidi idadi halisi ya wananchi waliojiandikisha katika vituo hivyo.Kwa hiyo matukio hayo na kasoro hizo zinabaki kuibua maswali mengi kwa watu wengi.
Maswali hayo yanayoibuka ndani ya vichwa vya watu wengi ni kwanini  jeshi la polisi lilitumia nguvu kubwa  kukamata wananchi na viongozi wa upinzani na kuvamia ofisi za vyama vyao  pasipo sababu za msingi na walifanya hivyo kwa malengo yapi na kutumwa na nani?. Na inakuaje kasoro nyingi, mfano namba ya wapiga kura kuzidi namba halisi ya watu waliojiandikisha katika vituo hivyo?Je chombo husika yaani tume hawakuwa wamejiandaa kukabiliana na aina ya udanganyifu wowote, au tume iliamua kufumbia macho kasoro hizo kwa kuweza kukibeba chama kilichokuwa madarakani?
Kama Afrika tumeamua kukubali mfumo wa vyama vingi basi tuwe tayari kukabiliana na matokeo ya mfumo huo,ni dhahiri na imezoeleka kuwa vyama vinavyokuwa madarakani  pale uchaguzi unapokaribia kufanyika matukio mengi yamekuwa yakijitokeza,yaani serikali iliyopo madarakani kutumia kila njia kutaka kushinda uchaguzi kwa kukiuka taratibu na kujenga taswira machoni  mwa watu kwa  vyama vya upinzani  kuonekana kama  chanzo cha vurugu katika chaguzi.
Nafikiri  ifike pahala watawala watambue kuwa vyama vya upinzani vinaweza kuongoza nchi kama wananchi wameamua kuvipa ridhaa,hivyo maamuzi hayo yaheshimiwe kwa sababu wananchi ndiyo wenye nchi na ni jukumu lao kuamua nani atakuwa kiongozi wao, isitumike nguvu kubwa ya chama tawala kutumia nguvu dora kuhakikisha uamzi wa watu unaingiliwa.Tumeamua kuruhusu mfumo wa vyama vingi,hivyo tuwe tayari kukubali matokeo ya mfumo huo.
Chagulani,Shabiru

25.2.2016