3/31/2015
Kulikoni Ughaibuni : Kwanini naunga mkono #CyberCrimeBill (Muswada wa k...
Kulikoni Ughaibuni : Kwanini naunga mkono #CyberCrimeBill (Muswada wa k...: Pengine kabla ya kueleza kwanini naunga mkono muswada wa kudhibiti uhalifu wa mtandaoni (The Cyber Crime Bill),ni vema nikaeleza backgr...
3/18/2015
Je,serikali inawajibika?
Je, serikali inawajibika?
Serikali katika misingi ya kidemokrasia ujipatia viongozi wake kupitia uchaguzi unaofanyika sehemu
husika.Viongozi hao wanaochagulia ndio baadae utengeneza serikali katika ngazi
mbalimbali ili kuweza kutimiza majukumu ya kiserikali.Viongozi hawa ndiyo wanaokua
wawakilishi wa wananchi katika shughuli mbalimbali za kiserikali, pia Kiongozi
kama rais naye ufanya uteuzi wa watu
mbalimbali ili waweze kumsaidia katika idara mbalimbali kiutendaji ili kuweza kufikia malengo kwa maendeleo na ustawi wa nchi
husika.
Hivyo serikali
yenye kujua na kutambua wajibu wake ujikita zaidi kwa kuwajibika ili kuweza kuhudumia wananch kwa kutumia
rasilimali ilizonazo na kuwahakikishia ustawi uliokua mzuri kimaisha.Hivyo
wananchi ujenga imani na serikali yao kwa
kuona serikali ikiwahakikishia ustawi wao katika Nyanja mbalimbali kama
za kijamii na kiuchumi.
Na serilikali
zilizokua makini na zenye malengo ya dhati hutekeleza majukumu yao kwa kuhakiki
wananchi mfano wafanya biashara wanapata mazingira mazuri yakuwezewsha biashara
hizo kufanyika kwa urahisi na mazingira rafiki, hivyo watu hawa uweza kujipatia
kipato kupitia biashara zao na kuweza kuendesha familia zao na pia serikali
ukusanya kodi kwa wafanya biashara hawa.
Kodi inayopatikana
kama mapato hutumiwa na serikali katika kuendesha shughuli zake kwa kutoa
huduma kwa wanachi mfano kama upatikanaji wa vifaa tiba na mdawa
hospitalini ili kuweza kuhudumia wagonjwa kwa kuhakikisha huduma za afya
zinapatikana kwa urahisi.vilevile
wananchi watataraji kupata huduma za maji ili kuweza kurahisisha shughuli
zao na pia watatarajia serikali inahakikisha uwepo wa elimu bora kwa uwepo wa
watalam, mazingira bora yakufundishia na vifaa bora vya kufundishia .
Upatikanji
wa huduma hizo muhimu kwa wananchi utekelezwa na serilali yenye ni ya dhati
kuona taifa linapiga hatua kimaendeleo katika nyanja mbalimbali .lakini kwetu
hapa mambo yamekua tofauti na jinsi wananchi walivyotaraji kua uwepo wa
serikali madarakani kuwa ni heri kwa mfano baada ya uchaguzi kufanyika serikali
uonekana kama vile inasahau wajibu wake mfano katika elimu mazingira ya
kufundishia saio rafiki, vifaa vya kufundishia hakuna hali hii upelekea utendaji kazi katika sehumu
hiyo kuwa mgumu na hatimaye ufaulu ushuka na elimu pia ushuka hili lipo wazi
kwa matokeo ya kidato cha nnea yaliyopita yalikua mabaya na hatujaona hatua
zilizochukuliwa ili kutatua tatizo hili.
Katika afya pia huduma bado ni duni hasa
katika upatikanaji kwa maana ya vituo kuwa
mbali hasa maeneo ya vijijini ambapo wananchi ulazimika kutembea umbali
mrefu kili kuweza kupata huduma .Na hata
wakifika vifaa tiba hakuna hivyo hali hii upelekea vifo hasa kwa mama
wajawazito wanaotembea umbali mrefu kutafuta huduma hizo huko vijijni,na mijini
vuilevile huduma ni duni madawa na watalaam
hakuna hii nayo uwafanya wataalam kutofika vituo vya kazi maana mazingira sio
rafiki na hatimaye kimbilio lao ni nje ya nchi. Mfano Botswana ndio limekua
kimbilio la madaktali wengi kutoka Tanzania.
Upatikanaji wa
maji nalo ni kero kwa wanachi mijini na vijijini pia. Vijijini watu usafiri
umbali mrefu wakati wa usiku hasa akina
mama ili kuweza kupata maji kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli mbalimbali za
nyumbani.MIjini pia maji nayo ni ya mgao na sehemu nyingine hayapatikani kabisa
wananchi ulazimika wakati mwingine
kununua maji kwa gharama kubwa,kutopatikana kwa maji upelekea kukwama kwa
shughuli za uzalishaji hata za nyumabani pia,tatizo hili lipo maeneo mengi hasa
Dar es salaam,Morogoro,Singida na
Dodoma.
Umasikini nao
umezidi kuongezeka kwa wananchi kila kukicha.Hi inatokana na serikali kutotumia
rasilimali ilizonazo ili kuwatengeneza wananchi fursa ili nao waweze kujiinua
kimaisha, na badala ake serikali kuwanyanyasa wananchi pale wanapojishughulisha
kwa kuanzisha biasharara ndogondogo kwa
kuwatoza kodi bila kuwaboreshea mazingira salama kwa ajili ya kuendesha
shughuli zao na wakati mwingine wajasiriamali hao ufukuzwa na serikali bila
hata kutafutiwa sehemu nyingine ya kuweza kueendeshea buiashara zao. Hali
upelekea watu kutokua na uhakika hata wa kupata kipato cha kuweza kumudu maisha yao
Ni jukumu la
serikali kuakikisha wananchi na mali zao wanakua salama kupitia mamlaka
zake.Kwetu hapa usalama wa raia uko mashakani
hii ipo wazi na linadhihirishwa na matukio mengi ambayo yamekua
yakitokea hapa nchini watu kupotza uhai na hata mali zao pia, mfano hivi majuzi
tumempoteza Dr Sengondo Mvungi aliyevamiwa nyumbani kwake huko kibamba. Pia malalamiko mengi yamekua yakitolewa juu ya
utendaji wa jeshi la polisi kukamata watu ovyo na pengine mtu kutosikilizwa na
hatimae jeshi la polisi ufikia uamzi wa kufanyanya lolote lile kwa jinsi litakavyo
dhidi ya raia.
Serikali makini
kote duniani ukemea vikali masuala ya rushwa. Hapa kwetu ni tofauti kidogo kwa
maana ya mamlaka husika uonekana kua wakali kwa matukio madogo madogo ya rushwa
lakini mamlaka hizi ushindwa kutekeleza wajibu wake pale tuhuma za rushwa dhidi
ya viongozi wa umma zinapotokea na hatua uchukua muda mrefu kuchukuliwa kwa
kisingizio cha uchunguzi unafanyika . Mfano
tuhuma mbalimbali zimekua kikitolewa juu ya baadhi ya viongozi wa serikali lakini hakuna chochote kinachofanyika .Hali
hii upelekea kushamiri kwa vitendo hivyo kama ilivyo sasa.
Serikali makini inapopata ridhaa ya kuwa madarakani, jukumu
lake kubwa ni kuhakikisha ustawi wa
wananchi wake unakua bora ili kuweza
kupiga hatua kimaendeleo katika nyanja zote na sio kufikiria uchaguzi mwingine
pale wanapo pewa na ridhaa na wananchi.
Chagulani Shabiru
Mwanza, Tanzania
2014
Je kodi inakusanywa ipasavyo ili kuleta maendeleo?
Je kodi inakusanywa ipasavyo ili
kuleta maendeleo?
Ni dhahiri
kua serikali yoyote duniani ili iweze kuendeshwa lazima ihakikishe wananchi
wanalipa kodi mbalimbali kuwezesha
shughuli za serikali kufanyika, ikiwemo kuhudumia wananchi wake katika
huduma mbalimbali mfano maji,afya,elimu na kadhalika .
Ni miezi
mitatu imepita kodi ya laini ya simu(sim
card tax) imepitishwa na serikali, na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) imeziandikia barua kampuni za simu kuzitaka kuanza kukata kodi hiyo kwa kila mtumiaji
mwenye laini ya simu,hivyo ( TRA ) imeagiza kukata kodi kuanzia mwezi wa saba
mpaka sasa kwa maana mwananchi hana budi kulipa shillingi elfu
tatu .Taifa lolote ili liendelee lazima likusanye kodi kama vyanzo vya mapato
katika kuendesha shughuli mbalimbali za serikali hivyo kila mwananchi hana
wajibu wa kulipa kodi kwa maana ya kuwa mfanyakazi ,mfanyabiashara kutokana na
biashara au kazi afanyayo na kodi nyingine ukusanywa na kulipwa kupitia
manunuzi ya bidhaa mbalimbali .
Mapato yanayokusanywa na serikali kupitia kodi mbalimbali serikali haina budi kuyarudisha kwa
wananchi kwa kuhakikissha wananchi wanapata huduma bora katika elimu,maji , afya
na huduma nyingine. Mfano kupitia kodi inayokusanywa na serikali tunategemea
katika vituo vya afya madawa na
vifaa tiba viwepo ili kuwezesha wananchi kupata matibabu kwa urahisi lakini kwetu hapa huduma zimeendelea kuwa
duni kila kukicha hasa maeneo ya vijijini
kutokana na mamlaka husika kutotekeleza
wajibu wake katika ukusanyaji wa kodi kama vyanzo vya mapato kwa serikali.
Hali hii ya kutokuwepo dhana ya uwajibikaji
katika mamlaka husika zilizopewa dhamana ya kuhakikisha kodi inalipwa
inapelekea wafanyabiashara wakubwa na hata makapuni makubwa kutokulipa kodi ipasavyo na hata yakilipa kodi ni kwa kiasi
kidodo ukilinganisha ukubwa na uzalishaji wa makampuni hayo, na wafanya
biashara wadogowadogo wamekua wakilipa kodi lakini hawatengezewi miundo mbinu
itakayowawezesha biashara yao kua
endelevu na hatimae hunyanyaswa kwa kufungiwa
biashara zao na wakati mwingine uendesha shughuli zao katika mazingira yasiyo
rafiki
Wakati mwingine umekuwepo misamaha ya
kodi kwa makampuni tajiri ya madini wakati makampuni haya yamekua
yakipata faida kubwa sana kupita kiasi na kukataa kueleza wazi mapato
wanayoyapata mfano makapumpuni ya simu
yamekua hayalipi kodi inayotakiwa ukilinganisha na faida inayopatikana kupitia
mitandao hiyo ya simu.
Hali hii inatokana na mamlaka husika
kutotokeleza wajibu wake ipasavyo na
kutokuwepo kwa uadilifu katika ukusanyaji wa mapato hasa kwa makampuni makubwa
kama ya simu na migodi pale maafisa wa mamlaka hizo wanapotengewa kiasi kikubwa
cha fedha na makampuni hayo na hatimae kiasi kidogo ukusanywa na mwisho wa siku
mzigo uelekezwa kwa mwanachi wa kawaida( mlalahoi) asiyekua na uhakika wa kupata hata milo miwili kwa siku,mwananchi huyu atake
asitake lazima alipie kadi ya simu yake kwa kila mwezi kama serikali
ilivyoelekeza kupitia mamlaka ya mapato Tanzania.inasikitisha sana kuona
wafanyabiashara wakubwa wenye kumiliki makampuni makubwa pia wanakwepa kulipa kodi kutokana na
ushawishishi wa kifedha walio nao .
Serikali za
mataifa yaliyoendelea duniani yamejidhatiti zaidi katika ukusaji wa kodi
kwa uadilifu na uzalendo ili kuweza kupata mapato yatakayowezesha serikali
kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wake lakini kwetu hapa wajanja wachache
wamejidhatiti katika kukwepa kodi na kuruhusu mianya ya rushwa ili zoezi la ukusanyaji wa kodi kutofanyika kama inavyotakiwa na hali hii
huzolotesha kasi ya maendeleo kwa taifa
pale serikali inapojikuta ikikopa
pesa nje kwa ajili ya bajeti.
Chagulani Shabiru
Mwanza,Tanzania
2014
Tusitarajie katiba mpya kwa sasa
Katiba ni
mwongozo wenye sheria na kanuni mbalimbali kwa ajili ya uendeshaji wa
nchi.Mataifa yaliyo makini duniani uruhusu
utaratibu uliokuwa bora kwa kuwashirikisha wananchi katika upatikanaji
wa katiba kwa kukusanya maoni yao na kuyafanyia uchambuzi kupitia tume na kisha
katiba kutungwa kwa kuzingatia maoni yaliyopendekezawa na wananchi.
Katika mchakato wa kutafuta katiba mpya mh rais
aliteua tume iliyokusanya maoni na kuyafanyia uchambuzi wa kina na badae
likawepo bunge maalum la katiba ambalo lilijumuisha wajumbe mbali mbali kama wabunge wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania ambao walipatikana kwa sheria iliyopitishwa na bunge nao kuwa sehemu
ya bunge maalum la katiba, na wajumbe wengine ni kutoka vyama vya siasa,asasi
zisizo za kiraia ambao waliteuliwa na
Rais.
Baada ya uteuzi wa wajumbe wa bunge maalum la katiba
,kazi yao kubwa ilikua ni kusimamia
rasimu kwa kujadili maoni yaliyotolewa na wananchi na kuyaboresha pia. Suala la kusimamia maoni ya wananchi
kwenye rasimu linaonekana kutozingatiwa, hili linadhihirishwa kwa baadhi ya vifungu vilivyoko kwenye rasimu
kuodolewa ,mfano ni kifungu kilichokuwa kikizungumzia tunu za taifa ambazo ni
uadilifu,uzalendo na uwajibikaji.Kifungu hiki kimepuuzwa na wajumbe kutoka
chama tawala, na hali hiyo ilipelekea umoja wa katiba ya wananchi ( UKAWA) na baadhi ya
wajumbe wengine kutoka bungeni kwa kutoridhiswa na mwenendo wa bunge .
Na kuanza kwa awamu ya pili kwa bunge maalum la
katiba kumetiliwa shaka hasa ukizingatia baadhi ya wajumbe waliotoka nje hapo
awali, kwa kutoridhishwa na jinsi bunge lilivyokuwa likifanya kazi na jitihada
za kuhakikisha wajumbe hao kurejea bungeni zikigonga mwamba kutokana na
kutofikiwa kwa maridhiano kwa pande zote
mbili,Hali hii imepelekea upande mmoja yaani wajumbe ambao ni sehemu kubwa ya
Chama cha Mapinduzi wao kuonekana ndiyo wenye dhamana ya kuhakikisha katiba
inapatikana.
Uwepo huu wa idadi kubwa ya wajumbe ambao ni sehumu
ya chama tawala kuendelea na bunge maalum unatiliwa shaka,hii nikutokana
wajumbe hao kuondoa kifungu cha wananchi kuwajibisha mbunge na ukomo wa
ubunge,kitendo hiki kinaashiria wajumbe kulinda maslahi binafsi kwa kushindwa
kusimamia maoni ya wananchi kwa kuyaboresha na badala yake wanaondoa vifungu
ambavyo vinaonekana kwao vinaweza kuwa havina maslahi,kufanya hivi ni kinyume
na jukumu la bunge maalum la katiba.
Kwa hatua hii bunge kutawaliwa na hisia na kushindwa
kujikita katika kujadili maoni ya wananchi ni kiashiria tosha kuwa uwezekano wa
kupata katiba bora iliyotokana na maoni
ya wananchi ni mdogo,hii ni kutokana na hali halisi inayoendelea kwa baadhi ya
wajumbe kuwa nje ya bunge na mjadala ukiendelea bungeni na waliobaki bungeni
kutotimiza majukumu yao na badala yake mchakato kutekwa na msimamo wa chama na
wakati mwingine hali hii kuonekana kama fursa kwa baadhi ya wajumbe kama
washindi ( winners) kwa kuendelea kubaki bungeni na walioondoka kuonekana
kama walioshindwa ( losers)
Na historia inaonyesha udhaifu wa bunge letu kutumia wingi wao
kufanya maamuzi hata kama hayana tija kwa wananchi ilimradi yana maslahi kwa
chama kinachounda serikali, hivyo hii dhana ya winners na losers inaweza
kupelekea maamuzi kufanyika vibaya
ilimradi yaa tija kwa watawala,nadhani ungekuwa wakati mzuri sasa kwa
kujifunza kutoka kwa majirani zetu kama
Kenya walioweka tofauti zao pembeni na kutanguliza maslahi ya taifa mbele
katika upatikanaji wa katiba.
Mwisho kabisa,upatikanaji wa katiba ni maridhiano
kwa kuweka misimamo ya vyama pembeni na kusimamia rasimu iliyotokana na maoni
yalitolewa na wananchi na itakayodumu kwa miaka mingi ijayo .kutopatikana kwa
katiba itakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za wananchi zilizotumika kuendesha
bunge na kulipa posho wajumbe, na
wananchi watakuwa hawajatendewa haki kwa pesa zao kutumika vibaya .
Chagulani Shabiru
Kutoka St. Augustine, Mwanza.
2014
Subscribe to:
Posts (Atom)