3/18/2015

Je kodi inakusanywa ipasavyo ili kuleta maendeleo?



                            Je kodi inakusanywa ipasavyo ili kuleta maendeleo?
Ni dhahiri kua serikali yoyote duniani ili iweze kuendeshwa lazima ihakikishe wananchi wanalipa kodi mbalimbali kuwezesha  shughuli za serikali kufanyika, ikiwemo kuhudumia wananchi wake katika huduma mbalimbali mfano maji,afya,elimu na kadhalika .
Ni miezi mitatu  imepita kodi ya laini ya simu(sim card tax) imepitishwa na serikali, na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA)  imeziandikia barua kampuni za simu kuzitaka  kuanza kukata kodi hiyo kwa kila mtumiaji mwenye laini ya simu,hivyo ( TRA ) imeagiza kukata kodi kuanzia mwezi wa saba mpaka  sasa kwa maana  mwananchi hana budi kulipa shillingi elfu tatu .Taifa lolote ili liendelee lazima likusanye kodi kama vyanzo vya mapato katika kuendesha shughuli mbalimbali za serikali hivyo kila mwananchi hana wajibu wa kulipa kodi kwa maana ya kuwa mfanyakazi ,mfanyabiashara kutokana na biashara au kazi afanyayo na kodi nyingine ukusanywa na kulipwa kupitia manunuzi ya bidhaa mbalimbali .
   Mapato yanayokusanywa na serikali  kupitia kodi mbalimbali  serikali haina budi kuyarudisha kwa wananchi  kwa kuhakikissha wananchi  wanapata huduma bora katika elimu,maji , afya na huduma nyingine. Mfano kupitia kodi inayokusanywa na serikali  tunategemea  katika vituo vya afya  madawa na vifaa tiba viwepo ili kuwezesha wananchi kupata matibabu kwa urahisi  lakini kwetu hapa huduma zimeendelea kuwa duni kila kukicha hasa maeneo ya vijijini  kutokana na  mamlaka husika kutotekeleza wajibu wake katika ukusanyaji wa kodi kama vyanzo vya mapato kwa serikali.
 Hali hii ya kutokuwepo dhana ya uwajibikaji katika mamlaka husika zilizopewa dhamana ya kuhakikisha kodi inalipwa inapelekea wafanyabiashara wakubwa na hata  makapuni makubwa kutokulipa kodi  ipasavyo na hata yakilipa kodi ni kwa kiasi kidodo ukilinganisha ukubwa na uzalishaji wa makampuni hayo, na wafanya biashara wadogowadogo wamekua wakilipa kodi lakini hawatengezewi miundo mbinu itakayowawezesha  biashara yao kua endelevu na hatimae hunyanyaswa kwa  kufungiwa biashara zao na wakati mwingine uendesha shughuli zao katika mazingira yasiyo rafiki
  Wakati mwingine umekuwepo misamaha ya kodi  kwa makampuni tajiri  ya madini wakati makampuni haya yamekua yakipata faida kubwa sana kupita kiasi na kukataa kueleza wazi mapato wanayoyapata mfano  makapumpuni ya simu yamekua hayalipi kodi inayotakiwa ukilinganisha na faida inayopatikana kupitia mitandao hiyo ya simu.
         Hali hii inatokana na mamlaka husika kutotokeleza wajibu wake ipasavyo  na kutokuwepo kwa uadilifu katika ukusanyaji wa mapato hasa kwa makampuni makubwa kama ya simu na migodi pale maafisa wa mamlaka hizo wanapotengewa kiasi kikubwa cha fedha na makampuni hayo na hatimae kiasi kidogo ukusanywa na mwisho wa siku mzigo uelekezwa kwa mwanachi wa kawaida( mlalahoi)   asiyekua na uhakika wa kupata hata  milo miwili kwa siku,mwananchi huyu atake asitake lazima alipie kadi ya simu yake kwa kila mwezi kama serikali ilivyoelekeza kupitia mamlaka ya mapato Tanzania.inasikitisha sana kuona wafanyabiashara wakubwa wenye kumiliki makampuni makubwa pia  wanakwepa kulipa kodi kutokana na ushawishishi wa kifedha walio nao .
  Serikali za  mataifa yaliyoendelea duniani yamejidhatiti zaidi katika ukusaji wa kodi kwa uadilifu na uzalendo ili kuweza kupata mapato yatakayowezesha serikali kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wake lakini kwetu hapa wajanja wachache wamejidhatiti katika kukwepa kodi na kuruhusu mianya ya rushwa ili zoezi la  ukusanyaji wa kodi  kutofanyika kama inavyotakiwa na hali hii huzolotesha kasi ya maendeleo kwa taifa  pale serikali inapojikuta ikikopa  pesa nje kwa ajili ya bajeti.
     Chagulani Shabiru
    Mwanza,Tanzania
    2014

No comments:

Post a Comment