3/18/2015



                                            
                    Tusitarajie katiba mpya kwa sasa
 Katiba ni mwongozo wenye sheria na kanuni mbalimbali kwa ajili ya uendeshaji wa nchi.Mataifa yaliyo makini duniani uruhusu   utaratibu uliokuwa bora kwa kuwashirikisha wananchi katika upatikanaji wa katiba kwa kukusanya maoni yao na kuyafanyia uchambuzi kupitia tume na kisha katiba kutungwa kwa kuzingatia maoni yaliyopendekezawa na wananchi.

Katika mchakato wa kutafuta katiba mpya mh rais aliteua tume iliyokusanya maoni na kuyafanyia uchambuzi wa kina na badae likawepo bunge maalum la katiba ambalo lilijumuisha wajumbe mbali mbali  kama wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao walipatikana kwa sheria iliyopitishwa na bunge nao kuwa sehemu ya bunge maalum la katiba, na wajumbe wengine ni kutoka vyama vya siasa,asasi zisizo za kiraia  ambao waliteuliwa na Rais.

Baada ya uteuzi wa wajumbe wa bunge maalum la katiba ,kazi yao kubwa  ilikua ni kusimamia rasimu kwa kujadili maoni yaliyotolewa na wananchi na kuyaboresha  pia. Suala la kusimamia maoni ya wananchi kwenye rasimu linaonekana kutozingatiwa, hili linadhihirishwa  kwa baadhi ya vifungu vilivyoko kwenye rasimu kuodolewa ,mfano ni kifungu kilichokuwa kikizungumzia tunu za taifa ambazo ni uadilifu,uzalendo na uwajibikaji.Kifungu hiki kimepuuzwa na wajumbe kutoka chama tawala, na hali hiyo ilipelekea umoja  wa katiba ya wananchi ( UKAWA) na baadhi ya wajumbe wengine kutoka bungeni kwa kutoridhiswa na mwenendo wa bunge .
Na kuanza kwa awamu ya pili kwa bunge maalum la katiba kumetiliwa shaka hasa ukizingatia baadhi ya wajumbe waliotoka nje hapo awali, kwa kutoridhishwa na jinsi bunge lilivyokuwa likifanya kazi na jitihada za kuhakikisha wajumbe hao kurejea bungeni zikigonga mwamba kutokana na kutofikiwa kwa maridhiano kwa pande  zote mbili,Hali hii imepelekea upande mmoja yaani wajumbe ambao ni sehemu kubwa ya Chama cha Mapinduzi wao kuonekana ndiyo wenye dhamana ya kuhakikisha katiba inapatikana.
Uwepo huu wa idadi kubwa ya wajumbe ambao ni sehumu ya chama tawala kuendelea na bunge maalum unatiliwa shaka,hii nikutokana wajumbe hao kuondoa kifungu cha wananchi kuwajibisha mbunge na ukomo wa ubunge,kitendo hiki kinaashiria wajumbe kulinda maslahi binafsi kwa kushindwa kusimamia maoni ya wananchi kwa kuyaboresha na badala yake wanaondoa vifungu ambavyo vinaonekana kwao vinaweza kuwa havina maslahi,kufanya hivi ni kinyume na jukumu la bunge maalum la katiba.
Kwa hatua hii bunge kutawaliwa na hisia na kushindwa kujikita katika kujadili maoni ya wananchi ni kiashiria tosha kuwa uwezekano wa kupata katiba bora  iliyotokana na maoni ya wananchi ni mdogo,hii ni kutokana na hali halisi inayoendelea kwa baadhi ya wajumbe kuwa nje ya bunge na mjadala ukiendelea bungeni na waliobaki bungeni kutotimiza majukumu yao na badala yake mchakato kutekwa na msimamo wa chama na wakati mwingine hali hii kuonekana kama fursa kwa baadhi ya wajumbe kama washindi ( winners) kwa kuendelea kubaki bungeni na walioondoka kuonekana kama  walioshindwa ( losers)
Na historia inaonyesha  udhaifu wa bunge letu kutumia wingi wao kufanya maamuzi hata kama hayana tija kwa wananchi ilimradi yana maslahi kwa chama kinachounda serikali, hivyo hii dhana ya winners na losers inaweza kupelekea maamuzi kufanyika  vibaya ilimradi yaa tija kwa watawala,nadhani ungekuwa wakati mzuri sasa kwa kujifunza  kutoka kwa majirani zetu kama Kenya walioweka tofauti zao pembeni na kutanguliza maslahi ya taifa mbele katika upatikanaji wa katiba.
Mwisho kabisa,upatikanaji wa katiba ni maridhiano kwa kuweka misimamo ya vyama pembeni na kusimamia rasimu iliyotokana na maoni yalitolewa na wananchi na itakayodumu kwa miaka mingi ijayo .kutopatikana kwa katiba itakuwa  ni matumizi mabaya  ya fedha za wananchi zilizotumika kuendesha bunge na kulipa posho  wajumbe, na wananchi watakuwa hawajatendewa haki kwa pesa zao kutumika vibaya .
Chagulani Shabiru

Kutoka St. Augustine, Mwanza.
2014
  

No comments:

Post a Comment