Leo ni tarehe 9/12, ni siku kubwa sana kihistoria kwa Taifa letu.Ni siku
ambayo nchi yetu ilipata uhuru kutoka kwa wakoloni,harakati za
kupigania uhuru zikiongozwa na Mwl Julius K.Nyerere,harakati hizo
zilianaza punde baada ya vita ya pili ya dunia kwa mataifa ya yaliyokuwa
chini ya ukoloni,lengo lilikuwa ni Afrika kuwa huru na waafrika
kujitawala wao wenyewe,
Kimsingi, haikuwa kazi ndogo maana wengi waliweza kupoteza uhai kwa maana ya damu kumwagika na kuhakikisha Afrika inakuwa huru.Harakati hizo zilifanikiwa lakini kwa muda mrefu,hivyo lengo lilifankiwa na Afrika kuwa huru na watu wake kuwa huru.Kwa mara ya kwanza baada ya harakati hizo kufanikiwa,waafrika waliweza kijitawala kwa maana ya kuwa viongozi wa nchi na kuanza kujenga nchi zao kwa kutumia rasilimali zilizkuwepo Afrika na kuhakikisha kila mwafrika ananufaika na rasilimali hizo.
Lakini baada ya viongozi hao kutawala na baadae kustaafu tumeshuhudia mambo kutoenda sawa kwa maana ya waliokabidhiwa kijiti kubadilika na kuwa wakoloni weusi na waafrika kuanza kuonekana kama watumwa ndani ya nchi zao,hili linaweza kudhihirishwa na baadhi ya nchi za kiafrika kuwa mambo hayaendi sawa kwa mifumo iliyopo sasa kwa kutokuwepo kwa mgawanyo sawa wa rasilimali na waafrika kutofaidi rasilimali walizobarikiwa.
Wito wangu na kilichopelekea mimi kutoa mtazamo huu ni kuwakumbusha watawala wetu kuwa pale tunaposherekea uhuru,tusisherekee tu kwa gwaride na anasa kwa tabaka tawala bali tukumbuke lengo la kupigania uhuru yaani waafrika kuwa huru na kujitawala na serikali kusimamia rasiliamali zilizopo na kila mwafrika kunufaika na rasilimali hizo na kujenga mataifa yetu kwa ujumla.
Chagulani,Shabiru
09.12.2015
Kimsingi, haikuwa kazi ndogo maana wengi waliweza kupoteza uhai kwa maana ya damu kumwagika na kuhakikisha Afrika inakuwa huru.Harakati hizo zilifanikiwa lakini kwa muda mrefu,hivyo lengo lilifankiwa na Afrika kuwa huru na watu wake kuwa huru.Kwa mara ya kwanza baada ya harakati hizo kufanikiwa,waafrika waliweza kijitawala kwa maana ya kuwa viongozi wa nchi na kuanza kujenga nchi zao kwa kutumia rasilimali zilizkuwepo Afrika na kuhakikisha kila mwafrika ananufaika na rasilimali hizo.
Lakini baada ya viongozi hao kutawala na baadae kustaafu tumeshuhudia mambo kutoenda sawa kwa maana ya waliokabidhiwa kijiti kubadilika na kuwa wakoloni weusi na waafrika kuanza kuonekana kama watumwa ndani ya nchi zao,hili linaweza kudhihirishwa na baadhi ya nchi za kiafrika kuwa mambo hayaendi sawa kwa mifumo iliyopo sasa kwa kutokuwepo kwa mgawanyo sawa wa rasilimali na waafrika kutofaidi rasilimali walizobarikiwa.
Wito wangu na kilichopelekea mimi kutoa mtazamo huu ni kuwakumbusha watawala wetu kuwa pale tunaposherekea uhuru,tusisherekee tu kwa gwaride na anasa kwa tabaka tawala bali tukumbuke lengo la kupigania uhuru yaani waafrika kuwa huru na kujitawala na serikali kusimamia rasiliamali zilizopo na kila mwafrika kunufaika na rasilimali hizo na kujenga mataifa yetu kwa ujumla.
Chagulani,Shabiru
09.12.2015
No comments:
Post a Comment